Player_logo Podcasts Community Create a Podcast
125216651
460>_1070617

Mwishoni mwa juma nilipata nafasi ya kuzungumza na Mbunge wa Bariadi Mashariki Mhe. John Momose Cheyo (UDP) kuhusu suala la kampuni ya Meremeta ambayo imepokea mabilioni ya shilingi toka Benki Kuu na hakuna mtu aliye tayari kusema wazi kampuni hiyo ni ya nani.

Mahojiano yangu na Bw. Cheyo yalikuja masaa machacha baada ya majibizano yake na Waziri Mkuu Mhe. Pinda Bungeni siku ya Ijumaa ambapo alikataa kuyakubali maelezo ya Waziri Mkuu kuwa kampuni ya Meremeta na nyingine yenye kuhusiana nazo inahusiana na masuala ya Usalama wa Taifa.

Wakati huo huo tunarajia kurusha mahojiano yangu na Mhe. Chacha Wangwe na Bw. Tundu Lissu kufuata sakata ambalo limeanza kuibuka ndani ya Chadema. Mahojiano hayo yalifanyika masaa machache baada ya Kamati Kuu ya Chadema kumsimamisha Umakamu Mwenyekiti Bw. Wangwe kwa kukiuka maadili ya uongozi.

[PLAY]
460>_1062781

Habari ambazo zinapita pita kama vile maji ya mfereji zinasema kuwa Mhe. Karamagi anatarajiwa kuwa mkutano na waandishi wa habari hapo kesho, atakachozungumzia hakijajulikana bado na kama kinahusiana na masuala ya TICTS au masuala ya Richmond. Wakati huo huo Bunge linatarajiwa kutoa maamuzi kuhusu ombi la Dr. Mwakyembe kuhusu kanuni za Bunge.

Hii Alhamisi pia inatarajiwa Spika Sitta atatoa uamuzi wa kama kuruhusu Bunge lipige kura ya kutengua kanuni yake inayozuia kujadiliwa kwa azimio la Bunge au jambo lililotolewa uamuzi na Bunge hadi miezi 12 ipite. Endapo Bunge litaridhia kutengua kanuni hiyo, basi mjadala wa ripoti ya Kamati Teule ya kuhusu Kampuni ya Richmond utaanza tena Bungeni.

Mojawapo ya waliouhisika na sakata hilo wamesema kuwa wanaisubiri kwa hamu siku ambayo wataweza kujitetea mbele ya Bunge. "Hatukupata nafasi ya kujitetea, hivyo kanuni ikitenguliwa tutaweza na sisi kuelezea upande wetu" alisema mmoja wa Mawaziri ambao walijiuzulu kufuatia kashfa ya Richmond.

Hata hivyo, Dr. Mwakyembe na kamati yake wamesema wako tayari kusimama na kufafanua jambo lolote ambalo halikueleweka au kutoa hisia zao kuhusu yale ambayo yamekuwa yakifanyika. Kwa mujibu wa mjumbe mmojawapo wa Kamati ile Teule, kitendo cha NEC na sasa Wabunge kujaribu kwa nguvu zote kuwasafisha na kuwatetea viongozi waliojiuzulu kina lengo moja tu nalo ni kuvuruga jitihada nzima za kurudisha fedha zilizolipwa Richmond na kuondoa mjadala kuhusu Dowans na kuufanya uwe unahusu Kamati Teule.

"Angalia ni nani aliyesimama kutetea kurudishwa kwa malipo ya mamilioni ya shilingi kila siku kwa Dowans? Angalia ni mjumbe gani wa NEC ambaye amesema anataka malipo yasimamishwe; hakuna!" alisema mjumbe huyo kwa jazba akizungumza na KLHN.

"Hili jambo halijafikia mwisho" alisema Mbunge mwingine ambaye anamwelekeo wa kuiunga mkono kamati teule.

Muda wote kesho KLHN itakuwa inakuletea taarifa kwa kadiri zinavyopatikana kufuatia maendeleo yoyote kuhusu masuala yote mawili ambayo yanahusiana.

460>_1040334
Tafadhali soma habari kamili kwenye http://www.klhnews.com Wakati huo huo tumeanza kutangaza "live" kama majaribio kwa kucheza muziki. Tunaomba feedback yako mahali popote unapotusikia na kama unatusikia vizuri, na hasa wale walioko Tanzania.
[PLAY]
460>_1031135

Leo ni siku ya Bajeti. Waziri wa Fedha Bw. Mustafa Mkullo anatarajiwa kusoma bajeti hiyo leo na hivyo kuonesha ni wapi tumefika toka mwaka uliopita na wapi tunataka kwenda katika mwaka ujao wa fedha.

Nimepata nafasi ya kupata nakala ya bajeti hiyo ambayo inapatikana hapa: http://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=1680&d=1213211256 Tafadhali copy and paste kwenye browser yako.

Nimatumaini yangu mtapata nafasi ya kuipitia kabla hamjaisikia.

[PLAY]
460>_1028925
Bila ya shaka mlolongo wa matukio kadha wa kadha unaweza kumfanya mtu yeyote kushika tama na kukata tamaa. Hasa inapotokea matukio ambayo yanaihusu nchi yetu. Msururu wa kashfa ambazo zimeiandama nchi na viongozi wetu bila ya shaka vinaweza kukufanya ujisikie mpweke na mnyonge na zaidi kuweza kujiuliza "Tanzania ina matatizo gani?".

Kwa wengine kujiuliza swali hili kunaendana na hisia ya kuachwa peke (abandonment) na kukata tamaa (despair). Na zaidi ya yote kuna wengine ambao wanaweza kujihisi kuvunjwa moyo (discouraged) na hivyo kuona kuwa hakuna lolote na chochote kinachoweza kufanyika Tanzania ambacho kinaweza kuturudisha kwenye matumaini?

Je huu ndio wakati wa kukata tamaa na kuwaachia mafisadi wafanye wapendavyo? Je huu ndio wakati wa kukubali viongozi wabovu na wasio na uwezo alimradi tuendelee katika hali ya utulivu, amani na mshikamano? Je huu ni wakati wa kusalimu amri na kukubali kile ambacho kimetuangukia na kuwa yote ni "mapenzi ya Mungu"?

Je unajihisi kukata tamaa ukiangalia mambo yanayoendelea katika nchi yetu?

[PLAY]
460>_1005830

Baada ya miezi ya maneno, kejeli na hadi kuzomewa hatimaye Rais Mstaafu Bw. Benjamin Mkapa amezungumza wiki iliyopita akikanusha madai kuwa ametajirika visivyo halali. Zaidi ya yote amedai kuwa yeye anaishi kwa pensheni yake kama anavyoishi Mzee Mwinyi na yakuwa wanaozua maneno ya yeye kuwa "fisadi" ni watu ambao kwa maneno yake walitaka "awapendelee" alipokuwa madarakani na yeye "hakuwapendelea".

Na kabla wingu la utetezi wake huo halijatua kampuni ya Makaa ya Mawe ya Kiwira imejitokeza baada ya miezi kuhusishwwa na Urais wa Mkapa na kutangaza kuwa Rais Mkapa si mmiliki wa mgodi huo na hivyo kujaribu kuzima madai hayo. Hata hivyo mambo yafuatayo ni ya kuangalia na tuone kama utetezi wa Mkapa mwenyewe na Kiwira unatosha kumsafisha Rais Mstaafu.

Unaweza kusoma mjadala huu kwenye Jamiiforums.com mada ya "Kiwira yamsafisha Mkapa"

Tanpower Resources ilisajiliwa 29/12/2004 na kupewa namba 51080 ikiwa na dhumuni kuu la kwanza kuchimba mkaa wa mawe nakuzalisha umeme, wakati huo Mkapa bado ana hisa na alijua sababu za kuanzishwa kwake. Wakati inasajiliwa wanahisa walikua ANBEM hisa 200,000 na aliyesaini ni Anna Mkapa, Devconsult ya Yona na Mwanae (hisa 200,000), Universal Tech (hisa 200,000), Choice Industries ya Mbuna (200,000) na Fosnik Enterprises ya Nicholus Mkapa na mkewe Foster wakiwa wameiga jina la kampuni ya baba na mama zao ya ANBEM (wao wakiwa na hisa 200,000) na aliyesaini ni Nico

-----Lakini jambo la hatari ni kwamba, kabla hata ya TANPOWER kusajiliwa ilikwishaanza kufanya kazi na Evans Mapundi akiwa Mkurugenzi wake, alifanya mawasiliano Desemba 15 na wakatembelea Kiwira Desemba 18 na 20, kwa baraka za Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona. Yona akiwa pia mmoja wa wanahisa wa kampuni hiyo.

----Mkapa na Mkewe kupitia ANBEM walijitoa TANPOWER Februari 21, 2005 ikiwa tayari hata mkataba wa ubia kati ya TANPOWER na Kiwira umekwishaandaliwa na Yona akiwa Waziri wa Nishati na Madini.... Hata baada ya Kujitoa, Mwanae Nico na mkewe Foster na baba mkwe wao Mbuna walikua ndani ya Kiwira.

----Ni mwaka huo ambao Yona na bosi wake waliitosa STAMICO na kuchukua eneo jingine lenye hazina kubwa ya mkaa wa mawe liitwalo Kabulo rig ambalo serikali ilikopeshwa USD milioni 50 kufanya utafiti. STAMICO hadi sasa wanalilia eneo hilo ambalo limechukuliwa na TANPOWER/Kiwira bure

http://www.jamiiforums.com/photos/Mkapa1.jpg http://www.jamiiforums.com/photos/Mkapa2.jpg

SWALI

Je Umeridhika na utetezi na jitihada za kujisafisha za Rais Mkapa. Waandishi waache kumsakama Rais mstaafu kwa sababu Kiwira wamesema hahusiki nayo?

460>_995931

Tulikokuwa tunaenda siko, tumeamua kugeuka" - hayo ni baadhi ya maneno ya Mhe. Anne Kilango Malecela akizungumza na KLH News siku chache zilizopita akielezea mabadiliko ya wabunge wa CCM linapokuja suala la kulinda maslahi ya Taifa.

Kati ya mambo ambayo anayazungumzia ni pamoja na hali ya kisiasa nchini, kifo cha Ballali, kwanini wabunge wa CCM walikuwa wanaitetea serikali yao hata ilipokuwa inaharibu, kwanini anaamini Kikwete ni kweli anataka mabadiliko na masuala mengine kemkem.

Mahojiano yangu hayo na Mhe. Anne Kilango Malecela (CCM - Same Mashariki) yatarushwa siku ya Ijumaa kupitia KLH News International na pia tunatarajia yataweza kusomwa kwenye mojawapo ya magazeti ambayo yamekubali kutupa nafasi.

Mimi niko impressed na watu mara chache sana.. this is one of those times

[PLAY]
460>_985328
Hii ni marudio ya show tuliyofanya siku ya Jumapili. NI sehemu tu ya onesho hilo.
[PLAY]
460>_979164

What happened? why did it happen? do you have any idea who did it and why? do you believe it. What next!?

KLHN will air a Live Show on Sunday at 2:00PM EST (1:00PM CST, 9:00PM East African Time) to discuss the events that have transpired this past week especially the death that is shrouded in mystery and speculation of former Bank of Tanzania Dr. Daudi Thomas Said Ballali who passed away last Friday.

You can participate in the "live" show through a phone call in at 1 248 686 2010 during the live show, or you can call the same line through out Saturday and live your short message of your thoughts about the death and the events surrounding his passing.

Otherwise you can also write an email of not more than six lines paragraph to express your thought/s (anything more than that will be deleted) on the matter. Write to klhnews(at)klhnews.com

You can hear the show through http://www.bongoradio.com

Exclusive with this show is a suprise guest; an outspoken member of Parliament through CCM and a few other MPs from the ruling party and the opposition who will respond to the question posed to them on whether the death of Gov. Ballali should impact in anyway,shape or form the ongoing EPA investigation and how they received the news of his death.

This event is brought to you in association with JamiiForums and Bongo Radio.

NB: I know people can type and scream behind their computers and show their anger through the speed of their fingers.. it is about time to be heard.. let us hear that anger, frustrations, concerns etc.. don't be scared that they might know who you are.. it is about time to be heard, I know I will...

NOTICE: Any Tanzania Radio Station or media House that would like to stream or air this "live" show you are most welcome to do so just let us know so that we can acknowledge your listeners and identify your station.

DARING TO BOLDY GO, WHERE NO ONE ELSE DARE TO!

460>_930306
Aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Dr. Daud Balali amefariki dunia. Habari ambazo zimeanza kusikika tangu jana jioni na kuthibitishwa na ndugu zake zimesema kuwa Gavana Balali amefariki mwishoni mwa juma na mipango ya mazishi inafanywa. Anatarajiwa kuzikwa huko huko Marekani. Inatarajiwa taarifa ya kifo chake kutangazwa Tanzania baadaye leo. Sikiliza matangazo kuhusu kifo hicho hapa au kwa kutwa nzima ya kesho tutakuwa tunaleta maendeleo yoyote ya habari hii kwenye tovuti yetu ya http://www.klhnews.com ambako "we bring the news first".
[PLAY]

Next Page